Hot Widget

Type Here to Get Search Results !

Jinsi ya kupata Mb's za bure kila siku

Internet imekua ni muhimu sana kwa vijana wa ki-Tanzania katika maisha yao ya kila siku lakini wakati huo huo imekua ikipanda bei kadri siku zinavyozidi. Ni kawaida kuambiwa umepata unlimited internet access kwa mwezi baada ya kufanya malipo yasiyopungua elfu 35. 

Cha kushangaza ni kwamba baada ya muda mfupi wa matumizi hasa utafikia 3GB basi hapo huanza kua slow kwa siku zote zilizosalia. Hili si jambo zuri kwani kwa vijana kudownload, kuangalia muvi online na bila kusahau Youtube ndio habari hasa kuhusu Internet. Kifupi kitu chochote chenye Ukubwa zaidi ya 50MB kimsingi hua kama hakiwezekani tena kwa kutumia vifurushi tununuavyo kwa kuhofia spidi kupungua ama kugoma kufungua tena. 

Kama kuna kumdhibiti mtu asipate kwa kiwango anachotarajia basi kwa nini usimpe bure! PdProxy na internet fasta itamuwezesha mtu mwenye matumizi yasiyozidi 100mb kwa siku kuweza kutumia huduma hii bure kila siku. Iwapo utafauata maelekezo yafuatayo kwa umakini na kufanikiwa kuinstall hicho kijisoftware basi utakua umejiweka katika nafasi nzuri ya kupata 100MB bure kila siku kwa kutumia DEMO Server za PdProxy. 

FAIDA Internet hii itakuwezesha: kuona content zilizozuiwa kwa kawaida na ISP ama zile maalumu kwa nchi fulani - utaweza kuziona pia. Hakuna mtu ataweza kujua IP adress yako ama mahali ulipo. Hakuna hata hacker atakayeweza kubaini website gani unaperuzi ukiwa unatumia PD-Proxy.

 INAKUWAJE Kwa kua na modem yako inayokubali line ya Vod Tanzania isiyokua na pesa lakini ikiwa umeunganishwa, kwa msaada wa PDProxy uliyoinstall kwenye kompyuta yako basi utaweza kuperuzi Internet yenye kasi kama kawaida. MAHITAJI Modem inayokubali Line Ya Vod na line ya Vod Akaunti ya PDProxy Installation ya PdProxy kwenye kompyuta yako. Najua una shauku la kutaka kujua jinsi ya kuinstall ili uanze kutumia huduma hii.


HATUA YA KWANZA | KUJIUNGA - 

i) USAJILI
Hatua ya kwanza ni kujiunga na akaunti na huduma hii.
1. Signup kwa ajili ya kua na Akaunti ya PdProxy - fuata link hii: http://www.pdproxy.com/signup.htm 

ii) UTHIBITISHO
Hakiki akaunti Yako (Confirm Your Account) - baada ya ku-signup nenda kwenye email yako ili kuhakiki akaunti yako ya PdProxy .
Kwenye Inbox Yako utakuta email kutoka PdProxy na hakiki kwa kubofya linki iliyoandikwa Confirm  
my account now 

Baada ya hapo utakua umeshajipatia akaunti yako ya PdProxy. Hifadhi vizuri Username yako pamoja na password yako kwani ndizo zitakazotumiaka kwenye ile software baada ya kufuata haya maelekezo ya kuiinstall.


HATUA YA PILI | KUINSTALL PDPROXY SOFTWARE KWENYE LAP/KOMPYUTA


i) Download PD-Proxy Software


Download Download kijisoftware cha PD-Proxy kupitia link hii

Baada ya kudownload unatakiwa kudoble click hilo file ambalo litakua katika format ya WinRAR.
Ukidoble click hilo file na litafunguka  
highlight folder lililo ndani bila kulifungua na bofya Extract to 


 Chukua file ambalo utakua umelixtract na likopi.

Baada ya kulikopi, ingia local file drive C kama picha inavyoonesha.


Baada ya kua umelikopi na kuingia local drive C, ingia tena Program Files.


Lipest ndani ya Program Files na fungua folder hilo kwa kuli-double click

Right -click file lililoandikwa "PD-Proxy.exe" na li-run kama Administrator. Angalia picha hapo chini.

Start PD-Proxy Image

Uki-run as administrator PD-Proxy itajaribu ku-install TAP-Win32 driver. Na itafungua kama mfano wa taswira iliyo hapo chini. 

Searching TAP Driver

Kisha chini ya sekunde 10 mfano wa tafsira ya picha iliyopo hapo chini itatokea na kama haikutokea basi system yako itakua imeshainstall hizo TAP-Win32 kupitia software zingine. 
  
Kama picha hiyo itatokea kukutaka kuinstall hizo drivers ubofye "Install" kuendelea kuinstall na subiri kwa sekunde 10 installation imalize. Isipotokea si mbaya kwani utakua umeshaistall kupitia software zingine.

Installing TAP Driver

Utaona picha ifuatayo ifuatao kama umefanikiwa kuinstall vizuri TAP-Win32 driver. Kama usipotokea jaribu hizi hatua mara tatu zaidi na kama zitakua bado hazitokea basi ingia kwenye  ukuraasa huukwa maelekezo zaidi.


TAP Driver Installed

Sasa unaweza kuunga kwenye servers za DEMO kwa kupata 100MB za bure kila siku na kama utahitaji kuperuzi bila kikomo - baada ya malipo ya sh. elfu 10 kwa mwezi utaweza kuchagua server zingine zote. Ni kuchagua tu server unayotaka kutumia.

Server selection

Hakikisha protocol ili kujiunga ni lazima iwe UDP kwa spidi nzuri na uimara wa mtandao.

Protocol selection

Ingiza jina lako/username na password. Kama bado hujafungua akaunti yako basi ingia kwenye kurasa hii na ufuate maelekezo rahisi kutengeneza akaunti yako ya PD-Proxy .

Enter username and password

Enter username and password

Anza kwa kuunga modem yako yenye line ya vod isiyokua na pesa ama bando.
Kisha ukishaunga - fungua PdProxy yako na ubofye kwenye kitufe kilichoandikwa connect. Spidi ya mtandao huu utategemea sana spidi ya kompyuta yako na modem kwa wakati huo.


Kama windows firewall itakua enabled, windows itauliza kama unataka kuiruhusu PD-Proxy VPN kuunga  internet. Bofya kitufe cha "Allow access". 
Allow PD-Proxy in Firewall

Kama ukiona ujumbe huu kama picha ya chini inavyoonesha basi inamaanisha tayari umeshaungwa na mtandao na server za PdProxy. 

Ili kufikia hatua hii unatakiwa uwe umeunga modem yako yenye laini ya vod na ndipo uunge PdProxy software. Kwenye hizo field kama unataka kutumia 100mb za bure kwa siku basi utachagua server ya demo na kama utataka ile ambayo ni unlimited kwa siku 30 utatakiwa kulipia elfu 10.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Below Post Ad